Psalms 37:12-17


12 aWaovu hula njama dhidi ya wenye haki
na kuwasagia meno,

13 bbali Bwana huwacheka waovu,
kwa sababu anajua siku yao inakuja.


14 cWaovu huchomoa upanga
na kupinda upinde,
ili wawaangushe maskini na wahitaji,
kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.

15 dLakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe,
na pinde zao zitavunjwa.


16 eBora kidogo walicho nacho wenye haki
kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;

17 fkwa maana nguvu za waovu zitavunjwa,
lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.

Copyright information for SwhKC